Text: | Bwana nasikia kwamba |
Author: | E. Cordner |
1 Bwana nasikia kwamba
umebariki wengi,
nami nakuomba sasa:
Nibariki na mimi!
Na mimi na mimi
Nibariki na mimi.
2 Nipitie Baba yangu,
kweli mimi mkosaji,
Baba uingie kwangu,
nirehemu na mimi!
Na mimi na mimi
Nirehemu na mimi.
3 Nipite, nakuomba,
Bwana Yesu Mwokozi,
wakosaji wawaita,
uniite na mimi!
Na mimi na mimi
Uniite na mimi.
4 Nipitie Roh mwema
kweli mimi sioni,
mwenye nguvu za kuonya,
nipe nguvu na mimi!
Na mimi na mimi
Nipe nguvu na mimi.
5 Nipite Baba yangu,
nakuomba kwa bidii,
umebariki wengine,
ni bariki na mimi!
Na mimi na mimi
Nibariki na mimi.
Text Information | |
---|---|
First Line: | Bwana nasikia kwamba |
Title: | Bwana nasikia kwamba |
Author: | E. Cordner (1800) |
Language: | English |
Publication Date: | 1988 |
Topic: | Yesu anawapa wanfunzi wake Roho Mtakatifu |
Notes: | Sauti: Even me by Bradbury, 1816-1868, Sacred Songs and Solos #485, Augustana Hymnal #407 |