184. Bwana wetu umetoa

1 Bwana wetu umetoa
mara moja msalabani
mwili na maisha yako
kwa wokovu mtakatifu.

2 Ndiye kafara ya kweli
itoshayo siku zote;
kima chake ni kikubwa
hakiwezi kuzidishwa.

3 Mbinguni atuombea
akiwa kitini pake.
Na hapa atubariki,
tukila karamu yake.

4 Twaonyesha kufa kwake
mpaka atakaporudi;
tunaungana na yeye
kuwa viungo vyake tu.

Text Information
First Line: Bwana wetu umetoa
Title: Bwana wetu umetoa
German Title: Wir danken dir, Herr Jesu Christ
Author: C. Vischer (1600)
Language: Swahili
Publication Date: 1988
Topic: Chakula cha Bwana
Notes: Sauti: Herr Jesu Christ, wahr Mensch und Gott, Asili: Leipzig 1625, Posaunen Buch, Erster Band #20, Nyimbo za Kikristo #140
Tune Information
(No tune information)



Suggestions or corrections? Contact us