Text: | Bwana twakuomba sasa |
Author: | F. G. Klopstock, 1724-1803 |
1 Bwana twakuomba sasa:
Tutokee sisi hapa,
kwani siku yako leo.
Tupe, kufikiri vema
neno lako la uzima,
na la ukombozi wetu.
Sisi tuliopotea
tupate kurudi kwako.
2 Yawe mbali kwetu sasa
kila mambo masumbufu.
Roho na mioyo yetu
ikaongee na Mungu.
Tupate kutiwa hamu
ya raha iliyo kwako,
itakayotutokea
baada ya maisha haya.
3 Naona kitini pako
taji lao washindao;
nasikia nyimbo zao
waishao kupigana.
Hao wakusifu wewe
kwa zaburi na kwa shangwe.
Hata mimi nijalie
nipate kufika kule.
4 Upungufu wangu wote
ufunike wewe Bwana;
niwe mtakatifu wako
duniani hapa chini,
nisikose kuingia
furahani kwa wageni,
uliowaita wewe
kuimba nyimbo za shangwe.
Text Information | |
---|---|
First Line: | Bwana twakuomba sasa |
Title: | Bwana twakuomba sasa |
German Title: | Zeige dich uns ohne Hülle |
Author: | F. G. Klopstock, 1724-1803 |
Language: | Swahili |
Publication Date: | 1988 |
Topic: | Kumtambikia Mungu: Nyimbo za asubuhi |
Notes: | Sauti: Zeige dich uns ohne Hülle, Posaunen Buch, Erster Band #57 |