226. Naomba, Bwana ukae nami

1 Naomba, Bwana ukae nami,
ukija usiku sasa hivi.
Lakini kwako twaona mwanga,
ukae na mimi, jua bora.

2 Upesi kabisa siku zetu
zitapita, raha hatuoni.
Uharibifu uko popote,
ukae nami, umshinde mwovu.

3 Sitamwogopa tena Shetani,
ukiwa nami unibariki.
Sina mwingine ila wewe tu,
ukae nami hata usiku.

4 Ukae na mimi nikilala,
ukae na mimi nikiamka.
Unisikie Ee, Bwana Yesu,
Ukae na mimi mpaka mwisho.

Text Information
First Line: Naomba, Bwana ukae nami
Title: Naomba, Bwana ukae nami
English Title: Abide with me
Author: H. F. Lyte, 1739-1847
Language: Swahili
Publication Date: 1988
Topic: Kumtambikia Mungu: Nyimbo za Jioni
Notes: Sauti: Eventide by H. W. Monk, 1823-1889, Hymnal Companion #6, Nyimbo za Kikristo #177
Tune Information
(No tune information)



Suggestions or corrections? Contact us