121. Shujaa mkubwa

1 Shujaa mkubwa, Bwana wetu,
leo umejikalisha
kitini kwa Babako.
Ufalme wote ni wako,
umeshinda maadui,
hawanna nguvu tena.
Umepewa enzi kubwa,
kufa pia na uzima,
vyote unavitawala.

2 Malaika wote wa mbingu
wanakusifu kwa nyimbo,
wanakutumikia.
Ulipotoka mbinguni
ukaja kutuokoa,
na umerudi leo.
Sasa, wako utukufu;
nasi tunakushukuru,
tunasifu jina lako.

3 Twataka kutafuta tu
ufalme wako wa mbingu.
Utupe nguvu zako,
tushike mwenendo mwema,
tushiwe wenye kiburi
ila wanyenyekevu.
Tuepuke kila kosa,
tufuate njia yako
ya kuingia mbinguni.

4 Yesu mwana wa Daudi
uliyetupatanisha
na Bwana Mungu wetu.
Ulipokwenda mbinguni
umetutengenezea
makao ya milele.
Tuongoze, tusichoke,
tusafiri siku zote;
kwani watungoja kwako.

Text Information
First Line: Shujaa mkubwa
Title: Shujaa mkubwa
German Title: Ach wundergrosser Siegesheld
Author: E. Chr. Homburg, 1605-1631
Language: Swahili
Publication Date: 1988
Topic: Yesu amepaa mbinguni
Notes: Sauti: Wie schön leuchtet der Morgenstern by Ph. Nicolai, 1556-1608, Lutheran Book of Worship #43
Tune Information
(No tune information)



Suggestions or corrections? Contact us