Text: | Mwezi umechipuka |
Author: | M. Claudius, 1740-1815 |
1 Mwezi umechipuka
na nyota zamulika
mbinguni popote.
Makonde yote kimya,
na kunako mabonde
ukungu mzuri unakaa.
2 Dunia imekuwa
nchi ya utulivu,
ni nyumba ya raha.
Viumbe vyenye taabu,
waume, wake, wana
na watulie usiku.
3 Tukiwa na kiburi,
tu wakosaji sana,
wapuzi kabisa.
Twatunga vya uongo,
na maarifa yote
yametutenga na Mungu.
4 Utuonyeshe, Mungu,
wokovu wa kikweli,
tusijidanganye!
Tukae duniani
kama watoto wema
wamtegemeao Baba.
5 Na sasa ndugu zangu,
tuende kujilaza
kwa jina la Mungu.
Atupe usingizi
sisi tuliochoka,
hata majirani wote!
Text Information | |
---|---|
First Line: | Mwezi umechipuka |
Title: | Mwezi umechipuka |
German Title: | Der Mond ist aufgegangen |
Author: | M. Claudius, 1740-1815 |
Language: | Swahili |
Publication Date: | 1988 |
Topic: | Kumtambikia Mungu: Nyimbo za Jioni |
Notes: | Sauti: Der Mond ist aufgegangen by J. A. P. Schulz, 1767-1800, Nyimbo za Kikristo #181, Tumwimbie Bwana #32 |